KNH ILIPOKEA MAJERUHI 16 WA MAANDAMANO
Hospitali ya kenyatta ilipokea majeruhi 16 kufuatia maandamano ya hapo jana hapa Nairobi 7 wakilazwa na wengine 9 wakitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani.
Katika mkao na wana habari Daktari mkuu wa upasuaji katika hospitali ya Kenyatta Dr William Sigilai ameelezea hali ya mchuuzi aliyepigwa risasi na polisi na kusema amefanyiwa upasuaji ambapo waliondoa risasi na anaendelea kutibiwa.
Dkt Sigilai ameongeza kuwa wagonjwa wengine 2 wamefanyiwa upasuaji mmoja wao akiwa bado hajatambuliwa.
Imetayrishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































