BARAZA LA MAGAVANA KUCHAGUA VIONGOZI WAPYA LEO

Magavana 47 wa Kenya wanatazamiwa kuchagua uongozi mpya wa kuongoza Baraza la Magavana kwa muda wa miaka miwili ijayo.
Wakuu wa kaunti kwa sasa wanakutana katika uwanja wa Safari Park, Nairobi, ambapo pia watazingatia mpango mpya wa afya – Hazina ya Bima ya Afya ya Jamii na kuanzishwa kwake katika kaunti
Imetayarishwa na Janice Marete