#Sports

TUTAOGELEA KWA USHINDI KULE PARIS

Kocha wa Kenya wa kuogelea Fakry Mansoor na imani kua wachezaji wake Ridwan Abubakar na Maria Brunlehner watafuzu kwa nusu fainali ya Michezo ya Olimpiki ya Paris.

Akizungumza Alhamisi, alisema Abubakar amezidisha maandalizi yake kwa kushiriki katika mashindano ya vyuo vikuu nchini Uingereza kabla ya shughuli ya ziada katika mji mkuu wa Ufaransa.

Ridhwan Abubakar, ambaye ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu maarufu cha Bath, amekuwa akichapisha nyakati nzuri sio tu nchini Uingereza bali pia Ulaya.

Aliweka rekodi mpya ya kitaifa ya Kenya katika mbio za mita 400, ambapo alitumia 4:04.39, na kupata nafasi ya pili na kuvunja rekodi yake ya awali ya 4:05.65 katika Mashindano ya Kitaifa ya Kuogelea ya Međunarodno Plivačko nchini Croatia.

Katika Mashindano ya kuogelea ya Coimbra ya 2023 nchini Ureno, alishiriki katika mbio za mita 100 na 200, akitumia muda wa kuvutia wa 52.87 na 1:56.29, na baadaye akafunga pointi 696 na 674 za FINA mtawalia. Mansoor alisema Abubakar atashindana katika mbio za mita 400 zitakazoanza Julai 27. Abubakar alitarajiwa kujiunga na Miramas Camp mwishoni mwa juma.

Kwa upande wake, Brunlehner atakuwa na nia ya kuvunja rekodi yake ya kitaifa ya mita 50 ya saa 26:12, ambayo aliweka mwaka huu katika Mashindano ya Dunia yaliyofanyika Doha mwezi Februari.

Imetayarishwa na Nelson Andati

TUTAOGELEA KWA USHINDI KULE PARIS

WERE AGURA ZESCO

TUTAOGELEA KWA USHINDI KULE PARIS

AMADOU AJIUNGA NA VILLA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *