RAIS RUTO AENDELEA KUKWEA
Rais William Ruto ameendelea na ziara yake ya maendeleo kwa siku ya pili katika eneo la Mlima Kenya ambako amezindua miradi mbali mbali anayosema itasaidia kubadilisha Maisha ya wakazi wa eneo hilo.
Kaunti za Meru na Kirinyaga ni maeneo ambako Rais anazuru hii leo, akikariri kuwa urafiki wake na eneo hilo utasalia kuwa imara.
Rais ameandamana na naibu wake Kithure Kindiki na viongozi mbali mbali wa eneo hilo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































