E-GP SI TAFADHALI, RUTO AONYA
Rais William Ruto amesisitiza kuwa mfumo wa utoaji zabuni za serikali kwa njia ya kielektroniki yaani e-Procurement ni lazima, licha ya pingamizi kutoka kwa viongozi mbali mbali wakiwemo magavana na maseneta wanaosema shughuli za kaunti zimekwama kutokana na mfumo huo.
Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Rais Ruto amewakosoa wanaopinga mfumo huo, anaoutaja kuwa wenye kuhakikisha uwazi katika utumiaji wa fedha za mlipa ushuru.
Kulingana na wanaopinga, mfumo huo unachelewesha usambazaji wa vifaa kwa kaunti.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































