WAKENYA WAMIMINIKA JKIA
Huzuni imetanda katika uwanja waw a ndege wa kimataifa JKIA ambako maelfu ya wakenya wamewasili kusubiri mwili wa Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.
Wengi wa waliowasili wameonekana wakitokwa na machozi, baadhi wakiwa wamevalia nguo zenye picha ya kinara huyo wa ODM.
Matayarisho yanaendelea katika maeneo mbali mbali ambako mwili wa Odinga utapelekwa hii leo yakiwemo majengo ya bunge, bunge likijiandaa kutoa heshima za mwisho hii leo kuanzia saa nne asubuhi hadi usiku wa manane.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































