MGOMO WATATIZA UCHUKUZI KIRINYAGA

Shughuli za uchukuzi zimetatizika katika eneo la Kerugoya kaunti ya Kiriyaga, baada ya wahudumu wa matatu kugoma wakilalamikia hatua ya wamiliki wa magari ya kibinafsi kubeba abiria bila leseni.
Wahudumu hao wameapa kutorejesha magari yao barabarani hadi usimamizi wa kaunti hiyo utakapoingilia kati kutatua mgogoro huo.
Hata hivyo, maafisa wa polisi eneo hilo wamewataka wahudumu hao kurejelea shughuli zao wanaposhughulikia suala hilo
Imetayarishwa na Antony Nyongesa