RUTO AHIMIZA MAZUNGUMZO KUOKOA HALI UARABUNI
Rais William Ruto ameshutumu mashambulizi ya makombora yanayolenga ngome za kijeshi katika mataifa yaliyo mashariki ya kati huku vita vikichacha katika eneo hilo.
Haya yanajiri baada ya Iran, katika kulipiza kisasi dhidi ya uvamizi wa Amerika na Israel, kulenga ngome hizo katika mataifa ya United Arab Emirates, Qatar, Saudi Arabia, Oman, Iraq, Jordan, Kuwait na Bahrain.
Kupitia taarifa, Ruto amesema vita hivyo vinatishia usalama wa kimataifa, akihimiza mazungumzo yatakayopelekea kusitishwa kwa vita hivyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































