UOKOAJI WAENDELEA KWENYE MGODI KAKAMEGA
Familia za waathiriwa waliokwama kwenye vifusi baada ya kuangukiwa na ukuta wa mgodi wa dhahabu katika eneo la Shinyalu kaunti ya Kakamega zimehakikishiwa kuwa shughuli za uokoaji zitaendelea hadi wapendwa wao watakapookolewa.
Zoezi la uokoaji linaongozwa na maafisa wa usalama kwenye kaunti hiyo, wachimbaji migodi 12 wakihofiwa kukwama ndani ya mgodi huo.
Jumla ya wachimba migodi 20 walikuwa kwenye eneo hilo wakati wa mkasa huo wa jana jioni.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































