#Local News

ICHUNG’WA AMUENZI JOHANA NG’ENO

Kiongozi wa Wengi katika Bunge la Kitaifa, Kimani Ichung’wa, amemuenzi marehemu Johana Ng’eno akimtaja kama mwanasheria mahiri aliyetoa mchango mkubwa katika masuala ya kisheria ya Bunge.

Ichung’wa amesema Ng’eno alikuwa akishiriki kikamilifu katika mashauri ya kisheria, akiwashauri mawakili waliokuwa wakilitetea Bunge mahakamani kuhusu namna bora ya kuendeleza hoja zao.

Ichung’wa ameongeza kuwa historia ya mageuzi katika sekta ya makazi haitakamilika bila sura maalum kumhusu Johana Ng’eno

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *