MATOKEO NI YA WALIMU, SI WANAFUNZI- WAKAZI BUSIA
Wakazi wa Bumala kaunti ya Busia wamefanya maandamano kulalamikia matokeo duni yaliyorekodiwa na watahiniwa wa mtihani wa KCSE katika shule ya Bumala B, wakiulaumu usimamizi wa shule hiyo kwa matokeo hayo.
Wakizungumza baada ya maandamano, wakazi hao wameshinikiza mageuzi katika usimamizi wa shule hiyo.
Kwenye mtihani huo, shule hiyo ilipata alama ya wastani ya 3.23, watahiniwa wakiwa 122, watahiniwa 3 pekee wakipata alama ya kuwawezesha kujiunga na chuo kikuu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































