WANAFUNZI WALALAMIKIA KATEGORIA TATA
Hazina ya kufadhili elimu ya juu imepokea malalamishi kutoka kwa wanafunzi zaidi ya 10,000 wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu, wakisema wamewekwa katika kategoria ambazo haziwiani na mapato ya familia zao.
Mkurugenzi mkuu wa hazina hiyo George Munari amesema kuwa zoezi la kukagua malalamishi hayo litachukua muda wa wiki tatu.
Aidha, ametoa wito kwa usimamizi wa vyuo vikuu vya umma kuendelea kuwasajili wanafunzi wanaposubiria ufadhili kutolewa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































