TUREJESHE WANAFUNZI SHULENI RAIS RUTO AMESEMA

Rais William Ruto ametoa wito kwa wazazi kuwarejesha wanao shuleni akiwahakikishia kuwa mvua kubwa iliyosababisha uharibifu mkubwa na kupelekea kufungwa kwa shule kwa takribani wiki mbili imepungua.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa shule ya msingi ya Lenana jijini Nairobi Ruto amesisitiza kuwa serikali itaimarisha usalama wawanafunzi,walimu na wafanyakazi shuleni.
Ameongeza kuwa serikali kwa ushirikiano na bunge itakarabati madarasa na miundo msingi iliyoharibiwa na mafuriko.
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































