#Sports

TIMU YA CHUO KIKUU CHA PEERLESS KABARAK YAFANIKIWA KUFIKA FAINALI KATIKA MECHI ZA KUSF

Timu za michezo za Chuo Kikuu cha Kabarak ziliibuka kidedea wikendi katika michezo ya Shirikisho la Michezo la Vyuo Vikuu vya Kenya (KUSF) iliyoandaliwa katika Chuo Kikuu cha Laikipia, na kupata nafasi katika mashindano yajayo ya kitaifa licha ya kusitishwa ghafla kwa mashindano hayo kwa sababu ya usalama.

Katika kategoria ya mpira wa vikapu ya wanawake, timu ya Chuo Kikuu cha Kabarak ilipata ushindi mnono wa 50-23 dhidi ya Chuo Kikuu cha Maasai Mara katika nusu fainali, na kujikatia tiketi katika michuano ya kitaifa baada ya mapumziko ya miaka mitatu.

Ushindi huo ulijiri baada ya mfululizo wa maonyesho ya nguvu, ikiwa ni pamoja na ushindi wa 31-4 dhidi ya mwenyeji wa Chuo Kikuu cha Laikipia na ushindi mwingine wa 35-23 dhidi ya wapinzani wa chuo kikuu cha Egerton katika michezo ya pool.

Mercy Wanjiku aliongoza safu hiyo kwa alama 28, huku wachezaji wenzake Trazzy Amolo na Beryl Oyoo wakidondosha alama 5 kila mmoja. Kwa upande wa Maasai Mara, Rebecca Basele ndiye aliyeibuka kinara akiwa na pointi 9 kila mmoja.

Nahodha wa Wanawake wa Mpira wa Kikapu wa Kabarak Mercy Wanjiku alipongeza timu hiyo kwa uchezaji bora walioonyesha.

Imetayarishwa na Janice Marete

TIMU YA CHUO KIKUU CHA PEERLESS KABARAK YAFANIKIWA KUFIKA FAINALI KATIKA MECHI ZA KUSF

SIJAKUWA NA MSAIDIZI, RAIS RUTO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *