#Local News

MGOMO WA MADAKTARI KULEMAZA MATIBABU

Wakenya wanakabiliwa na hatari ya kukosa huduma za matibabu katika hospitali za umma iwapo serikali haitatekeleza matakwa ya madaktari ikiwemo nyongeza ya mishahara ndani ya muda wa siku 14 zijazo.

Wakitoa tangazo hilo, madaktari kupitia kwa katibu mkuu wa muungano wao Dakta Davji Atellah wameikosoa serikali kwa walichokitaja kama ukiukaji wa wazi wa mkataba wa maelewano wa kati ya mwaka 2017-2021.

Malalamishi mengine ni kutolipwa malimbikizi yao jinsi walivyokubaliana kwenye mkataba uliositisha mgomo wa mwaka jana.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

MGOMO WA MADAKTARI KULEMAZA MATIBABU

RUTO: TALAKA NA UCHINA HAIPO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *