WAZIRI MVURIA KWA AFRIKA: TUONGOZE VITA DHIDI YA MABADILIKO YA HALI YA ANGA

Taifa la Kenya kupitia waziri Salim Mvuria imetoa changamoto kwa mataifa ya Afrika kuwa katika mstari wa mbele katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuwekeza katika teknolojia ya kijani kibichi na nishati mbadala.
Waziri wa Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Salim Mvurya, katika hotuba yake kwenye mkutano wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA) mjini Kigali, Rwanda, amesema Afrika ina uwezo wa kuwa kinara wa kimataifa katika mapambano dhidi ya mabadiliko ya muda mrefu ya hali ya anga.
Imetayarishwa na Mercy Asami