#Local News

WAAKAZI WALALMIKIA UJENZI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU MAKONGENI.

Zaidi ya wakaazi 3,000 wa mtaa wa Makongeni hapa jijini Nairobi Nairobi wamelalamikia ubomoaji unaoendelea ili kupisha kujengwa kwa nyumba za bei nafuu kwenye ardhi ya ekari 139.

Hata hivyo baadhi ya wakaazi wamelalamikia fidia duni ambayo wanalipwa wakisema fedha hizo hazitoshi kugharamia mahitaji yao huku wengine wakiwa na tumbo joto ya masomo ya wanao mwaka ujao.

Aidha ni Zoezi ambalo linaendeshwa chini ya ulinzi mkali wa maafisa wa polisi,serikali ikisisistiza kuwa nyumba za bei nafuu ndio njia mwafaka na  suluhu kwa wananchi kupata makaazi bora.

Imetayarishwa na Jones Koikai

WAAKAZI WALALMIKIA UJENZI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU MAKONGENI.

KENYA NA MALASYIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *