NIKO TAYARI KUINGIA AUC, ODINGA
Ikiwa ni chini ya wiki moja kabla ya uchaguzi wa uwenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika AUC kuandaliwa, waziri mkuu wa zamani Raila Odinga ambaye pia ni moja kati ya wawaniaji 3 kwenye kinyang’anyiro hicho, amesema atakubali matokeo ya uchaguzi huo.
Akizungumza katika kongamano la viongozi wanawake wa chama cha ODM jijini Nairobi, Odinga hata hivyo amesema amejiandaa vya kutosha kwa ajili ya kuibuka mshindi.
Aidha, Odinga ameitaka serikali kukomesha visa vya utekaji nyara.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































