UGONJWA USIOJULIKANA MOMBASA WACHUNGUZWA
Wakenya na hasa wakaazi wa Mombasa wametakiwa kutokuwa na hofu serikali ikiendesha uchunguzi katika ugonjwa usiojulikana unaodaiwa kusababisha vifo vya watu 4 huko Migadini Mombasa.
Akiongea huko Kisumu mkurugenzi wa afya Dkt Patrick Amoth anasema uchunguzi wa awali umebaini kuwa waliofariki walikuwa pia wanaugua magonjwa mengine.
Naye waziri wa afya Aden Duale anasema chembe chembe kutoka kwa walioaga zinafanyikwa uchunguzi katika mahabara ya shirika la kemri huko Kilifi.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































