KENYA IMEJITOLEA KUTUMIA NISHATI MBADALA ILI KUKABILIANA NA MABADILIKO YA HALI YA ANGA.

Naibu Rais Rigathi Gachagua sasa amesema kuwa Kenya imejitolea kutumia nishati mbadala katika juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya anga.
Akizungumza wakati wa Kongamano la 9 la kila mwaka la kimataifa kuhusu Ufanisi wa Nishati, Gachagua amesisitiza dhamira ya Kenya ya kuendeleza ufanisi wa nishati, kulingana na Ajenda ya Afrika ya 2063.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kimataifa la Nishati (IEA) Dk. Fatih Birol, kwa upande wake amesikitishwa na matumizi makubwa ya nishati zisizo safi katika bara zima la afrika.
Imetayarishwa na Janice Marete.