#Local News

ALIYEKUWA MBUNGE WA KISUMU TOWN WEST KENN NYAGUDI AMEFARIKI

Aliyekuwa Mbunge wa Kisumu Town West, Kenn Nyagudi, ameaga dunia.

Nyagudi amefariki usiku wa kuamkia leo akiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta.

Spika wa Bunge la Kitaifa, Moses Wetangula, ameongoza viongozi kutuma risala za rambirambi, akiwapa pole familia na marafiki wa Nyagudi huku akiombea faraja kwa wapendwa wake.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *