9 WAFARIKI KWENYE AJALI NAIVASHA
Watu 9 wakiwemo Watoto wameaga dunia kwenye ajali ya barabarani kwenye barabara na Nakuru- Nairobi karibu na eneo la Kayole Naivasha baada ya basi la uchukuzi kugongana na gari dogo la uchukuzi aina ya Nissan.
Afisa wa idara ya upelelezi eneo hilo Isaac Kiama, amethibitisha ajali hiyo ya mapema leo, akisema mansura wanatibiwa katika hospitali ya Naivasha wakiwa na viwango tofauti tofauti vya majeraha.
Imearifiwa kuwa basi hilo lilikuwa likitoka eneo la Chwele kaunti ya Bungoma likielekea Nairobi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 


















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































