MASAIBU YA MOI HAYAISHI LEO- WAHADHIRI
Shughuli za masomo zimeendelea kutatizika katika chuo kikuu cha Moi, wafanyakazi na wahadhiri wakidai kutishiwa na usimamizi wa chuo hicho huku wakidai kuendelea na mgomo wao.
Wakizungumza wakati wa mkutano wao jijini Eldoret, wahadhiri hao wakiongozwa na katibu mkuu wa UASU tawi la Moi Busolo Wekesa wamesema wamepokezwa Zaidi ya nyaraka 20 kutoka kwa chuo kikiwataka warejee kazini.
Aidha, wamekanusha taarifa kwamba mahakama imewaagiza kusitisha mgomo wao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































