UPINZANI WAANZA ZIARA YA SIKU 5 MAGHARIBI, RIFT VALLEY

Viongozi wanaoegemea mrengo wa upinzani wameendeleza juhudu za kujitafutia uungwanji mkono kwenye uchaguzi mkuu ujao, wakiratibu misururu ya mikutano ya kisiasa na wakazi wa maeneo ya Magharibi na bonde la ufa. Mikutano hiyo ya wiki nzima inaanza hii leo katika kaunti 10, ikiongozwa na kinara wa DCP Rigathi Gachagua, Kalonzo Musyoka wa Wiper, Eugene Wamalwa […]

MAHAKAMA YAMWAMRISHA IG KANJA KUMWASILISHA BLOGA NDIANGUI

Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja ameagizwa na mahakama kuonyesha aliko bloga Ndiangui Kinyangia aliyetoweka siku 10 zilizopita. Kwenye uamuzi wake, jaji Chacha Mwita amemtaka Kanja kumwasilisha bloga huyo mahakamani bila kukosa au aseme ni kwanini hawezi kupatikana kifikia kesho saa tano asubuhi. Suala hilo litatajwa tena kesho. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KUNDI LA WAKENYA LAELEKEA MOSCOW KWA AJIRA

Kundi la wafanyikazi 50 raia wa Kenya waliondoka nchini wiki jana kwa fursa za ajira nchini Urusi, kuashiria mwanzo wa mpango mpya wa uhamiaji wa wafanyikazi unaolenga kushughulikia ukosefu wa ajira kwa vijana. Kundi hilo, linalowajumuisha watu kutoka kaunti mbalimbali, linatarajia kufanya kazi katika kiwanda cha kupakia chakula nje ya jiji la Moscow. Kulingana na […]

PSG WAMZIMA MESSI, INTER MIAMI

Klabu ya PSG ya Ufaransa imeibandua Inter Miami ya Lionel Messi kutoka mashindano ya FIFA Club World Cup yanayoendelea nchini Marekani, kwa kipigo cha mabao 4 bila jibu na kufuzu katika awamu ya robo fainali. Miami waliweka matumaini kwa nyota huyo wa Argentina kuwapa ushindi dhidi ya mwajiri wake wa zamani, ila mabingwa wa bara […]

NAIROBI UNITED WAINGIA AFRIKA

Mabingwa wa ligi ya NSL Nairobi United wamejikatia tiketi ya kushiriki mashindano ya kombe la mashirikisho ya bara Afrika yaani CAF Confederations, baada ya kutawazwa mabingwa wa kombe la FKF Cup hapo jana. Naibois ambao wamekuwa na mazoea ya kuwaangusha mababe wa soka nchini, waliwacharaza Gor Mahia kibano cha mabao 2:1 kwenye fainali za kombe […]

MWAMKO MPYA WA AFC LEOPARDS

Klabu ya AFC Leopards imepata mwamko mpya kupitia uongozi wa mchezaji wa zamani wa Harambee Stars Boniface Ambani, aliyechaguliwa hapo jana kuwa mwenyekiti wake, akiapa kuleta mageuzi katika usimamizi na uendeleshaji wa klabu hiyo. Ambani alijizolea kura 1,101, na kumbwaga Enos Mutoka aliyepata kura 682, Ambani akichukua hatamu za uongozi kutoka kwa mwenyekiti anayeondoka Dan […]

MAPEPO YA NHIF YAIHANGAISHA SHA

Changamoto za ufisadi zilizokuwa zikiikabili bima ya zamani ya afya NHIF zimeendelea kuikabili bima mpya ya SHA, serikali ikilaghaiwa takribani shilingi milioni 100 kupitia ulaghai unaoendelezwa kupitia ushirikiano wa hospitali na wagonjwa. Kulingana na ripoti, hospitali zimekuwa zikighushi maelezo ya wagonjwa na kudai malipo mara mbili, waziri wa afya Aden Duale akitangaza kufunga zaidi ya […]

MATIANG’I AHIMIZA MAZUNGUMZO

Waziri wa zamani Dr. Fred Matiang’i, amehimiza mazungumzo ya kitaifa kufanywa katika juhudi za kudhibiti machungu ya vijana na kurejesha mshikamano wa taifa. Kulingana naye, serikali imefeli kuwasikiliza vijana, hatua anayosema huenda ikaligawanya taifa. Naye kiongozi wa chama cha DCP Rigathi Gachagua, ameishutumu serikali kutokana na jinsi ilivyowashughulikia waandamanaji Jumatano iliyopita. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WABUNGE WATISHIA KUMBANDUA MURKOMEN

Wabunge wanaogemea mrengo wa aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua wametishia kuwasilisha bungeni hoja ya kumtimua kutoka mamlakani waziri wa usalama Kipchumba Murkomen kutokana na amri yake inayowataka polisi kuwafeytulia risasi wanaokaribia vituo vya polisi. Wakiongozwa na mbunge wa Manyatta kaunti ya Embu Gitonga Mukunji, wabunge hao wamesema amri hiyo inalenga kuendeleza mauaji ya kiholela. Hata […]

ODINGA ASHUTUMU ‘AMRI YA KUUA’ YA MURKOMEN

Kinara wa ODM Raila Odinga amemshutumu waziri wa usalama Kipchumba Murkomen kutokana na amri ya Murkomen ya kuwataka polisi wawapige risasi watakaokaribia kituo cha polisi, Odinga akiitaja amri hiyo kuwa ya kiholela. Akizungumza kwenye hafla moja katika eneo la Bondo, Odinga amemtaka Murkomen kuiheshimu sheria, inayowataka polisi kuwalinda raia Pamoja na mali zao. Hata hivyo, […]