BUNGE LAKUTANA KUIDHINISHA KUTUMWA KWA KDF
Bunge la Kitaifa limeandaa kikao maalum kuidhinisha ombi la Baraza la Ulinzi la kupeleka Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) huku kukiwa na maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha kote nchini.
Kulingana na Waraka wa Amri ya Ziada iliyopangwa leo, hatua hiyo itaambatana na Kifungu cha 241 cha Katiba kinachohitaji kuidhinishwa na Bunge kabla ya kutumwa kwa KDF kupitishwa.
Hoja hiyo ilipelekwa Bungeni baada ya ombi kutolewa na Baraza la Ulinzi siku hii leo.
Imetayarishwa Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































