MOFA WAPANIA KUPATA ALAMA TATU HII WIKENDI
Klabu ya MOFA inalenga kupata alama tatu watakapokutana na Fortune Sacco wikendi ijayo. Kocha wa MOFA, Charles Odero, anasema kuwa baada ya kuishinda Naivas, sasa ni muhimu pia kuwapiku Fortune, kwani analenga kumaliza katika nafasi tatu bora kwenye ligi hiyo msimu utakapotamatika.
MOFA ambao wako katika nafasi ya tano wakiwa na alama 38, alama 14 nyuma ya viongozi wa ligi Nairobi United, watawalika Fortune Sacco siku ya Jumamosi katika Kaunti ya Kisumu.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































