#Local News

KANU KUKATA RUFAA BAADA YA ‘KUPOKONYWA’ KICC

Chama cha KANU kimetangaza kukata rufaa uamuzi wa mahakama kuu kuamua kwamba ardhi ya jumba la mikutano KICC inamilikiwa na serikali na wala si chama hicho.

Katika taarifa saa chache baada ya uamuzi wa mahakama, KANU imesema haijaridhishwa na uamuzi huo, na kutangaza kwamba imewaagiza mawakili wake kukata rufaa.

Awali, jaji Jacqueline Mogeni ameamuru kwamba KANU ilipata ardhi hiyo kwa njia haramu, na kuongeza kwamba kwenye Ushahidi wao, KANU imeshindwa kuonyesha jinsi ardhi ya umma ilitengwa na kupewa mwenyekiti wa chama cha kisiasa

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *