WIZARA YA AFYA YAANZISHA UCHUNGUZI KUHUSU KIFO MUKUMU
Wizara ya Afya imeanzisha uchunguzi kuhusu kifo cha mama mjamzito kilichotokea katika hospitali ya kimisheni ya Mukumu, Kaunti ya Kakamega.
Akizungumza mbele ya kamati ya bunge, Waziri wa Afya Aden Duale amesema wizara inafuatilia chanzo cha kifo cha Grace Wambui Misigo baada ya familia kudai kuwa wauguzi katika hospitali hiyo walimdhulumu wakati wa kujifungua hadi akafariki.
Waziri Duale amesema uchunguzi wa kina utafanyika ili kubaini ukweli na hatua stahiki zichukuliwe.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































