UPANZI WA MICHE KUREJESHA HADHI YA MSITU MT. ELGON

Serikali inapania kurejesha hadhi ya msitu wa Mlima Elgon ulioko kwenye kaunti ya Bungoma na Trans Nzoia kwa kupanda miche milioni 10 katika kipindi cha miaka 5 ijayo.
Akizungumza na wanahabari, naibu mkurugenzi wa idara ya misitu Charity Munyasia amesema miche hiyo itapandwa kwenye ekari 7 za ardhi ya msitu huo.
Aidha, amesema kwamba mradi huo utatoa nafasi za ajira kwa wakazi walio karibu na msitu huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa