#Local News

WAZIRI MUTUA ATANGAZA KAZI NCHINI QATAR

Waziri wa Leba Alfred Mutua amekuwa akipokea msukosuko kutoka kwa umma kufuatia tangazo lake la nafasi za kazi kutoka kwa kampuni ya Qatar.

Sawa na bosi wake, Rais William Ruto, Mutua amekuwa mtetezi wa kusafirisha wafanyikazi wa ndani hadi mataifa ya kigeni ili kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira nchini Kenya ambacho kinafikia asilimia 12.7.

Katika tukio hili, Mutua amechapisha kwenye mtandao wake wa kijamii kuhusu kampuni ya Qatar ambayo maafisa wake wako Nairobi kutafuta wafanyakazi wenye ujuzi katika nyanja mbalimbali.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *