NIMENAWA MIKONO

Vikao vya kusikiliza hoja ya kumwondoa afisini Waziri wa kilimo Mithika Linturi kutokana na Sakata ya mbolea ghushi vimekamilika leo hii.
Mbunge wa Bumula Jack Wamboka ambaye ndiye aliyewasilisha hoja hiyo bungeni ameiomba kamati inayochunguza hoja hiyo kuhakikisha kwamba Linturi ameondolewa afisini.
Akiwasilisha hoja yake ya mwisho mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na mbunge maalum Naomi Waqo,wamboka amesema wakenya wengi hasa wakulima wanakadiria hasara kutokana na utepetevu wa Waziri Mithika Linturi.
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































