MKURUGENZI WA WHO AITISHA MKUTANO WA DHARURA

Mkurugenzi mkuu wa shirika la afya duniani WHO Dkt.Tedros Adhanom Ghebreyesus ataitisha kamati ya dharura kufuatia ongezeko la ugonjwa wa M-pox,
Mkutano huo unatarajiwa kutoa mwelekeo iwapo mkurupuko huo ni dharura ya afya ya umma ya kimataifa na ikiwa ni hivyo itatoa ushauri mapendekezo ya muda ya jinsi ya kuzuia na kupunguza kuenea kwa ugonjwa huo.
Mkutano huo unajiri baada ya AFRICA CDC kutangaza M-pox kuwa dharura ya afya ya umma katika bara hili.
Imetayarishwa na Janice Marete