RUTO AMWAGIZA IG KUMALIZA UHUNI
Macho yote sasa yameelekezwa kwa idara ya polisi kuanzisha msako na kuwakamata washukiwa wa uhuni ambao wamekuwa wakivuruga mikutano ya kisiasa kote nchini, mwathiriwa wa hivi punde akiwa aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua Jumapili iliyopita.
Akitoa amri yake, Rais William Ruto amemwagiza Inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kuhakikisha washukiwa wote wanakamatwa ili kulihakikishia taifa utulivu.
Naye Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen, amesema magenge hayo hayatavumiliwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































