WAUGUZI WASITISHA MGOMO TRANS NZOIA
Huduma za matibabu katika hospitali za umma kaunti ya Trans Nzoia zinatarajiwa kurejelea hali ya kawaida hii leo kufuatia kusitishwa kwa mgomo wa wauguzi ambao umedumu kwa zaidi ya mwezi mmoja.
Hatua hiyo imejiri kufuatia mazungumzo ya kina kati ya muungano wa wauguzi KNUN na serikali ya kaunti hiyo, KNUN ikiongozwa na katibu mkuu tawi hilo Edward Cheruiyot ikisema mwajiri wao amekubali kutekeleza matakwa yao kikamilifu.
Aidha, Cheruiyot amesema muungano huo utafuatilia utekelezaji wa makubaliano hayo ili kuhakikisha wanachama wanasaidika wanapowahudumia wagonjwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































