NAIBU RAIS RIGATHI GACHAGUA AWAHAKIKISHIA WAKAAZI WA LAIKIPIA USALAMA

Naibu wa rais Rigathi Gachagua amewataka maafisa wa usalama katika kaunti ya Laikipia kuimarisha usalama katika kaunti hiyo.
Kwa mujibu wa Gachagua rais William Ruto amejitolea kutimiza ahadi aliyotoa ya kumaliza utovu wa usalama katika kaunti hiyo ya Laikipia.
Ameogeza kuwa serikali imeweka mikakati ya kukomesha visa vya uvamizi wa wanyamapori karibu na mbuga za wanyama.
Imetayarishwa na Janice Marete