TAASISI ZA UMMA ZATAKIWA KUPUNGUZA MATUMIZI

Mwenyekiti wa kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa Ndindi Nyoro ametoa wito kwa taasisi za umma kutafuta namna ya kupunguza gharama ili huduma muhimu za umma zipewe kipaumbele kwa kutengewa bajeti.
Kwa mujibu wa Nyoro kamati ya fedha Pamoja na hazina ya Taifa wanatafuta namna ya kuainisha matumizi ya fedha za umma ikiwemo kupunguza posho za wabunge.
Imetayarishwa na Janice Marete