#uncategorized

MOTO WATEKETEZA MALI YA THAMANI ISIYOJULIKANA EASTLEIGH

Mali yenye thamani isiyojulikana imeteketea baada ya moto unaokisiwa kutokana na kuvuja kwa mtungi wa gesi katika soko la Moonlight mtaani Eastleigh jijini Nairobi.

Wazima moto katika serikali ya kaunti ya Nairobi wamesaidia katika kuuzima moto huo.Akithibitisha kisa hicho, kamanda wa polisi kaunti ya Nairobi Adamsom Bungei amesema kuwa hakuna majeruhi ambao wameripotiwa.

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *