IEBC: HAKUNA WAPIGA KURA WAPYA
Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imepuzilia mbali madai kwamba wapiga kura wapya wamesajiliwa katika maeneo kutakakofanyika chaguzi ndogo hapo kesho ili kufanikisha wizi wa kura, ikisema hakuna wapiga kura wapya walio na uwezo wa kushiriki zoezi hilo.
Afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo Marijan Hussein Marijan, amekariri kuwa sajili itayotumika ni ile ya mwaka 2022.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































