#Local News

IAN NJOROGE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMSHAMBULIA POLISI

Dereva mmoja aliyemvamia na kumjeruhi afisa wa polisi wa trafiki huko Mirema jana Jumapili anatarajiwa kufikishwa mahakamani hii leo

Mshukiwa huyo kwa jina Ian Njoroge, amenaswa nyumbani kwake eneo la Jacaranda mtaani Kayole jijini Nairobi wakati wa operesheni iliyoongozwa na maafisa wa upelelezi DCI

Kwa mujibu wa polisi afisa kwa jina Jacob Ogendo alikuwa akidhibiti msongomano wa magari katika barabara hiyo alipolisimamisha gari moja lililokuwa limekiuka sheria za trafiki na liliposimama Ogendo alimwagiza dereva huyo kuandamana nae hadi kituo cha polisi kabla ya kumshambulia.

Imetayarishwa na Janice Marete

IAN NJOROGE AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMSHAMBULIA POLISI

SALASYA ATAKA MIRADI ILIYOKWAMA IKAMILISHWE

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *