WAZEE WA MITAA KUJUA HATMA
Hatma ya wasimamizi wa vijiji kuanza kupokea malipo yao ya kila mwezi itabainika hivi karibuni kutokana na maoni yatakotolewa na wakenya kwenye vikao vya ukusanyaji wa maoni vinavyoongozwa na wizara ya usalama wa kitaifa.
Vikao hivyo vitaandaliwa hapo kesho katika kaunti 10 ikiwemo Kakamega, Nairobi, Uasin Gishu, Nakuru, Mombasa na Machakos.
Kwenye pendekezo hilo, wazee hao ambao kwa sasa wanafahamika kama village elders, watapewa wadhifa wa village administrative elders.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































