#Local News

BADO HATUELEWANI NAIBU GAVANA ODUOL ASEMA

Naibu gavana wa kaunti ya Siaya William Oduol ameiambia kamati ya ugatuzi katika bunge la seneti kwamba uhusiano wake na gavana James Orengo umedorora tangu jaribio la kubanduliwa kwake mwezi juni mwaka jana.

Amesema kwamba mara kwa mara serikali ya kaunti hiyo imemhujumu kwa kukosa kumpa marupurupu yake na fedha zingine za kumwenzesha kutekeleza majumu yake.

Kamati hiyo hata hivyo imeahidi kusikiliza upande wa gavana Orengo kabla ya kujaribu kuwapatanisha.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *