DIDMUS- GACHAGUA ATAKUWA RAIA DISEMBA
Mbunge wa Kimilili kaunti ya Bungoma Didmus Barasa, amesema kwamba naibu rais Rigathi Gachagua atabanduliwa kutoka mamlakani kabla ya Disemba mwaka huu.
Akihutubu katika eneo bunge lake, Barasa amesema hatua ya kumbandua Gachagua imechochewa na uamuzi wake wa kueneza siasa za kikabila mwaka jana na kulifananisha taifa na kampuni ya wenye hisa.
Hata hivyo, wandani wa Gachagua wameapa kupinga hatua yoyote ya kumtimua.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































