WAUGUZI BUNGOMA WAANZA MGOMO, WAWATAKA WAGONJWA WAONDOKE

Baadhi ya wakazi katika kaunti ya Bungoma wametatizika kupata huduma za kimatibabu katika vituo vya umma kwenye kaunti hiyo kufuatia mgomo wa wauguzi wanaolalamikia madai ya kutotekelezwa kwa mkataba wao.
Wakizungumza mjini Bungoma, wauguzi hao wamelalamikia mazingira duni ya kazi, wakishikilia kwamba hawatarejea kazini hadi malalamishi yao yatakapoangaziwa.
Miongoni mwa matakwa yao ni ajira ya kudumu na nyongeza ya mshahara.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa