AJIUA BAADA YA KUUA

Polisi katika Kaunti Ndogo ya Nyatike wameanzisha uchunguzi kuhusu kifo cha mvulana wa umri wa miaka mitatu anayedaiwa kuuawa na babake, ambaye kisha alifariki kwa kujitoa mhanga huko Magungu, Kaunti ya Migori.
Akithibitisha kisa hicho naibu wa Chifu eneo hilo Zacheus Odero amesema uchunguzi wao wa awali umethibitisha kuwa mvulana huyo alichapwa viboko na babake wakati wa pambano lililozuka kati yake na mamake.
Alipogundua kuwa amemuua mwanawe, mtu huyo alijinyonga ndani ya nyumba.
Imetayarishwa na Janice Marete