RAIS RUTO APINGA KESI ZA GACHAGUA
Hatma ya naibu rais aliyetimuliwa Rigathi Gachagua imechukua mkondo mpya, baada ya Rais William Ruto kuwasilisha kesi mahakamani akisema kuwa mahakama kuu haina mamlaka ya kusikiliza kesi zinazopinga kutimuliwa kwa Gachagua.
Kupitia wakili wake Adrian Kamotho, Rais amepinga kesi iliyowasilishwa na David Mathenge na wengine 4 katika mahakama kuu ya Kerugoya, Rais akisema ni mahakama ya upeo pekee ndio yenye uwezo wa kusikiliza kesi hizo.
Haya yanajiri wakati ambapo Gachagua anasubiri kusikilizwa kwa kesi hizo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































