APOSTLE MANYURU AITAKA SERIKALI KUJUKUMIKA
Wito umeendelea kutolewa kwa serikali kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi ikiwemo kuweka mikakati itakayohakikisha utendakazi mwafaka kwa wananchi.
Wa hivi punde kutoa wito huo ni mwenyekiti wa Muungano wa Pentecostal Voice of Kenya PVK, Apostle Peter Manyuru, akiitaka serikali kuchukua hatua haraka za haraka kuhusu madai ya ufisadi kwenye Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA), ili kuimarisha sekta ya afya.
Akizungumza na wanahabari, Manyuru ambaye pia ni kiongozi wa kanisa la JTM, ameisistiza haja ya viongozi kuzingatia utendakazi kwa wakenya.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































