IEBC: RUTO APUUZA MAHAKAMA
Mwenyekiti mteule wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC Erastus Ethekon na makamishna 6 wa tume hiyo wanatarajiwa kuapishwa muda wowote ili kuanza rasmi majukumu yao baada ya Rais William Ruto kuwateua rasmi kuongoza tume hiyo.
Kwenye gazeti rasmi la serikali, Rais Ruto amewateua Anne Nderitu, Moses Mukhwana, Mary Sorobit, Hassan Noor, Francis Odhiambo na Fahima Abdallah.
Hata hivyo, uteuzi huo umefanywa licha ya agizo la mahakama kumzuia Rais Ruto kufanya hivyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































