MAAFA YA MAANDAMANO
Watu 8 wameripotiwa kuaga dunia huku wengine zaidi ya 400 wakijeruhiwa hapo jana kwenye makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wakiadhimisha mwaka mmoja tangu kuuawa kwa zaidi ya wakenya 60 wakati wa maandamano ya mwaka jana.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume ya kitaifa kuhusu haki za kibinadamu Dakta Raymond Nyeris, maafa hayo yaliripotiwa kwenye kaunti 6, watu 2 wakifariki katika ya Machakos saw ana Makueni, huku kaunti za Nakuru, Kiambu, Uasin Gishu na Nyandarua zikirekodi kisa kimoja mtawalia.
Aidha, tume hiyo imefichua kupokea taarifa za maandamano hayo kuingiliwa na makundi ya wahalifu.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































