LSK YAIPONDA IPOA
Rais wa chama cha wanasheria LSK Faith Odhiambo ameikosoa tume ya kucunguza mienendo ya maafisa wa polisi IPOA kufuatia tume hiyo kushindwa kuweka wazi ripoti yake kuhusu mienendo ya polisi wakati wa maandamano ya mwaka jana.
Akizungumza katika jumba la Ufungamano jijini Nairobi kwenye kongamano la LSK na mashirika ya kijamii kuwahamasisha vijana kuhusu haki zao na jinsi ya kupata haki, Odhiambo vile vile amemtaka Inspekta mkuu wa polisi Japheth Koome kung’atuka afisini.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































