DE LA FUENTE AKARIBISHA TETESI ZA KUSHINDA KOMBE LA DUNIA

Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis de la Fuente, amesema anafurahia shinikizo la kuwa miongoni mwa wagombea wakuu wa kushinda Kombe la Dunia, akizungumza kabla ya mechi ya kirafiki dhidi ya Misri jijini Barcelona. De la Fuente amempongeza nyota, Lamine Yamal, huku akiepuka kusema iwapo ataanza mechi dhidi ya timu ya Misri, ambayo […]

BONDIA OYOKO AFARIKI ULINGONI

Sekta ya ndondi nchini inaomboleza kufuatia kifo cha bondia Jacob Oyoko maarufu kama “Jack Spoiler”, aliyedondoka wakati wa pambano la kulipwa katika Ukumbi wa Utamaduni wa Mumias, Kaunti ya Kakamega. Kifo hicho kilithibitishwa na rais wa Tume ya Ndondi za Kulipwa nchini, Reuben Ndolo, aliyesema bondia huyo wa Kisumu alifariki licha ya kupatiwa huduma ya […]

STARLETS YATAJA KIKOSI CHA MUDA, SERENGE AITWA

Kocha wa Harambee Starlets, Beldine Odemba, ametaja kikosi cha muda cha wachezaji 31 kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ya wanawake yatakayofanyika Nairobi kuanzia Aprili 11 hadi 15, 2026. Kenya itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo yatakayofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Nyayo, yakishirikisha mataifa ya Australia, India na Malawi, huku wachezaji wakitarajiwa kuripoti kambini Aprili […]

KENYA YALIPA ADA YA AFCON

Baada ya wiki kadhaa za kutokuwa na uhakika, Kenya imelipa ada ya kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) yenye thamani ya dola milioni 30 (Sh3.9 bilioni), Waziri wa Michezo, Salim Mvurya, amesema kuwa nchi imetekeleza mahitaji yote yaliyowekwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Aidha ameongeza kuwa serikali imepanga upya Kamati ya Kuandaa Mashindano (LOC) […]

GACHAGUA AKOSOA UBOMOAJI GIKOMBA

Aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amelaani ubomoaji uliofanyika usiku katika soko la Gikomba, akiutaja kuwa usio na utu, wa kikatili na unaolenga kuwadhulumu wafanyabiashara wadogo. Akizungumza na wanahabari Jumanne, Machi 31, 2026, huko Makueni, Gachagua aliishutumu serikali kwa kupanga ubomoaji huo usiku, akisema hatua hiyo ni mateso kwa wananchi wanaojitafutia riziki. Alidai kuwa maelfu ya […]

SERIKALI YATOA HAKIKISHO LA MAFUTA

Waziri wa Nishati na Petroli, Opiyo Wandayi, amewahakikishia Wakenya kuwa nchi ina akiba ya kutosha ya mafuta licha ya mataifa kadhaa barani Afrika kukumbwa na uhaba. Akizungumza kufuatia taarifa za foleni ndefu katika vituo vya mafuta katika baadhi ya nchi, Wandayi amesema Kenya haijakumbwa na upungufu wowote na inaendelea kuwa na usambazaji thabiti wa bidhaa […]

GAVANA WATAKA HATI ZA KUKAMATWA ZIONDOLEWE

Baraza la Magavana limetaka kuondolewa mara moja kwa hati zozote za kukamatwa na hatua za shinikizo dhidi ya magavana, kukisubiriwa suluhu ya mzozo unaoendelea na Kamati ya Seneti ya Hesabu za Kaunti. Akizungumza na wanahabari Mwenyekiti wa baraza hilo, Ahmed Abdullahi, amesema hatua hiyo inalenga kulinda utaratibu wa kisheria na kuzuia kile alichokitaja kuwa kuingizwa kwa siasa […]

SENETI YAIDHINISHA MGAWANYO WA MAPATO

Kamati ya Kudumu ya Seneti kuhusu Fedha na Bajeti imeidhinisha ripoti yake kuhusu Mswada wa Mgawanyo wa Mapato kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027, hatua inayofungua njia kwa mjadala bungeni. Kwa mujibu wa taarifa ya Bunge iliyochapishwa hii leo, maseneta wamejadili athari za upungufu wa mapato ya kitaifa kwa serikali za kaunti. Kamati hiyo imebainisha kuwa ukusanyaji mdogo […]

KINDIKI AWATAKA MABALOZI KUITANGAZA KENYA

Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewataka mabalozi wa Kenya kuitangaza nchi kama salama na yenye fursa za uwekezaji, akisema ni jukumu lao kuvutia wawekezaji na wageni. Akizungumza wakati wa kufunga kongamano la 19 la mabalozi jijini Nairobi, Kindiki amesisitiza umuhimu wa mabalozi kushiriki kikamilifu katika kukuza taswira ya taifa kimataifa. Aidha ameongeza kuwa Kenya imepiga hatua kubwa […]

SILVA ATANGAZA KUONDOKA MAN CITY

Nahodha wa klabu ya Manchester City Bernardo Silva, amearipotiwa kuiarifu klabu hiyo kuhusu kuondoka kwake mwishoni kwa msimu huu. Kandarasi ya kiungo huyo raia wa Ureno mwenye umri wa miaka 31, itakamilika mwezi Juni mwaka huu, na ameonyesha ari ya kujiunga na klabu kadhaa bila ada yoyote. Silva alijiunga na City mwaka wa 2017, na […]